Psalms 57:1-3

Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni.

1 aUnihurumie, Ee Mungu, unihurumie,
kwa maana nafsi yangu inakukimbilia.
Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia
mpaka maafa yapite.

2 bNamlilia Mungu Aliye Juu Sana,
Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 cHutumana kutoka mbinguni na kuniokoa,
akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali;
Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
Copyright information for SwhNEN